MAAJABU YA DUNIA WAGHANA WAGEUZA MISIBA KUWA SEHEMU YA MBWEMBWE NA AJIRA!

Ukistaajabu ya Mussa autayaona ya Firauni,kama kawaida ya watu utofautiana kwa rangi,lugha,mila,desturi,tania na tamaduni basi ndivyo vivyo hivyo watu wametofautiana ktk kuchukulia uzito mambo mbalimbali ya kijamii ikiwemo sherehe na na misiba.

Huko ghana misiba imekuwa ni sehemu ya ajira muhimu sana kwa vijana baada ya ukosefu mkubwa wa ajira ktk nchi nyingi duniani,vijana hawa wamejiunga ktk kikundi cha watu wasiopungu 100 na kuunda kundi la kazi kwa ajili ya kuwafurahisha waliofiwa na ndugu zao hasa siku ya kuzika mwili wa ndugu zao.

Jamaa hawa wamekuwa wakifanya mbwembe za aina mbalimbali ktk umati wa watu ambao umekusanyika kabla ya mwili wa marehemu kusafirishwa au kuzikwa rasmi.

Ubunifu huu umewafanya vijana hawa kujipatia pesa kwa njia halali na kujitosheleza kimaisha.

Share :

Facebook Twitter Google+
0 Comments "MAAJABU YA DUNIA WAGHANA WAGEUZA MISIBA KUWA SEHEMU YA MBWEMBWE NA AJIRA!"

Back To Top