JE WAJUA SIRI ILIYOPO NDANI NA NJE YA INJINI ZA NDEGE! NI VITU GANI VIANAWEZA KUATHIRI UTENDAJI KAZI WAKE?

Ndege (EUROPLANE) ni mashine iliyogunduliwa kuanzia mnamo mwaka 1899 hadi ilipofikia 1903 ilikamilika na kufikia hatua ya kuruka angani agalau kwa kuwa na mtu mmoja,wataalam ndugu waliojulikana kama Wright brothers wao walifanikiwa kutengeneza ndege na kuirusha angani.

Usafiri huu muhimu na wa haraka zaidi unaweza kusafirisha watu na mizigo kutoka bara moja hadi jingine una siri nyingi zaidi ndani yake.

Ndege ni miongoni mwa usafiri salama sana lakini pia ndio usafiri wa hatari zaidi pindi inapotokea hitilafu ya kiufundi,hali ya hewa wakati ikiwa angani,kwanikuna kuwa na asilimia kubwa ya watu wote waliomo ndani kupoteza uhai wao.

Miongoni mwa matatizo hayo ni swala zima la kufeli kwa mifumo ya kiufundi hasa ya injini zake ambayo ndio chombo pekee kinachoifanya ndege kukaa angani,kutua au kuruka.

Pindi inapojitokeza hitilafu ya kiufundi itakayosabisha injini moja au zote uikiwa mbili au nne kulingana na ukubwa wa ndege yenyewe kuzima basi hapo tumaini la kusalimika huwa ni sawa na asilimia 0%

Injini za ndege ziko za aina na ukubwa tofauti na zinatengenezwa na makampuni mbalimbali kama Rolls Royce,General electric,Alliance na nyinginezo nyingi.

Ingini za ndege ziko za aina mbili yaani zile za awali ambazo mapanga yake ukaa kwa nje kama hizi za Bomberdier za kampuni ya huko Canada na zile za kisasa zaidi ambazo mapanga yake ukaa kwa ndani.

Injini hizi ambazo utengenezwa kwa ustadi wa hali ya juu zaidi na kisasa uwa na uwezo wa kunyanyua ndege kubwa za mizigo na abiria zenye tani nyingi zaidi ukilinganisha na zile za mapanga nje.

Ndege kubwa kama aina ya Airbus 380,Boing 737 zinatumia injini za Rolls royce trent xwb,alliance GP 7000,GE 9x 737,GE90-777,GE90-115B injini hizi huwa na uwezo wa nguvu za Horse powe HP hadi 50,000.

Injini moja inaweza kugahrimu dola za kimarekani milioni 13.5 hadi 35 hivyo kwa ndege za injini mbili au nne gaharama itakuwa zaidi ya hapo yaai mara mbilia ua mara nne .

Mfano kutengeneza ndege ya Airbus 380 moja tu inagharimu zaidi ya dola milioni 376 ikiwa sawa na shilingi bilioni 8,272,000,000 (bilioni nane milioni mia mbilia sabini na mbili) taslim.

Injini za ndege uathiriwa utendaji wake kazi na mambo yafuatayo:-

Kuingia kwa vumbi la milipuko ya kivolukano hasa ktk maeneo ya milima ya iana hiyo,vumbi na moshi wa volukano uathiri sana utendaji wa injini za ndege na uweza kufanya injini kuzima ghafla na kuleta madhara makubwa,ndege uzuiwa kupita maeneo ya hii au kuahirisha safari kabisa hadi pale kutakapotulia.

Kuingia kwa Ndege(Birds) ktk injini husika pia ni tatizo kubwa kwa injini kuweza kufeli kufanya kazi na kuifanya kusimama kabisa hivyo kuleta matatizo kwa chombo,mizigo na watu waliomo humo.

Kuishiwa kabisa kwa mafuta kabisa ni miongoni mwa tatizo kubwa litakalosababisha injini hizi kushindwa kufanya kazi kabisa,tatizo hili linaweza kuwa la makosa ya kibinadamu,usomaji mbaya wa kiasi cha mafuta kwa chombo maalum,kluapata dharura ya kupitia umbali mrefu usiokuwepo ktk ratiba,kushikiliwa na watekaji nyara (Plane hijackers) hivyokuiweka na kuipeleka ndege kusikokuwa rasmi,kuvuja kwa tanki ya mafuta au kufeli mifumo ya unyonyaji wa wa mafuta kwenda ktk injini.

Injini moja ya ndege huwa na matundu 16 hadi 20 (Nozzles or Valves) ya kuchomea mafuta,hii ufanya kwa baadhi ya injini kutumia mafuta mengi zaidi.

Ndege ina uwezo wa kusafiri kwa masaa 16-20 bila kutua sehemu aukuongeza mafuta tena.

Usukaji wa injini za ndege ni miongoni mwa mambo yanayotumia teknolojia ya hali ya juu sana.









Share :

Facebook Twitter Google+
0 Comments "JE WAJUA SIRI ILIYOPO NDANI NA NJE YA INJINI ZA NDEGE! NI VITU GANI VIANAWEZA KUATHIRI UTENDAJI KAZI WAKE?"

Back To Top