RIPOTI YA PILI YA MAKINIKIA:WALIO HUDUMU WIZARA YA NISHATI NA MADINI KUANZIA 1998 KUKIONA

Wafanyakzi wote waliofanya kazi kwa njia moja au nyingine ktk wizara ya nishati na madini kuanzia mwaka 1998 hadi sasa kufanyiwa uchunguzi na maohojiano ya kina na kamat maalum ya rais Magufuli ili kujibu shutuma na uzembe uliokuwa ukitendeka na wafanyakazi hao walikuwa na majukumu mbalimbai na Taasisi,vitengo kama TMAA kushindwa kukusanya kodi ya serikali ipasavyo,kuingia mikataba inayoumiza maslahi ya taifa na raia kwa ujumla.

Rais Magufuli ameagiza kamati hiyo kuendelea kuhoji na kutafutawatu wote na viongozi waliohusika kwa njia moja au nyingine waliingiza taifa ktk aina hii mbaya ya mikataba ya madini iliyopelekea taifa kupata hasara kubwa ya kukosa mapato makubwa ya matrilioni ya shilingi kwa kushindwa kukusanya kodi kikamilifu .

Baadhi ya mawaziri hawa waliowahi kuhudumu wizara hii na kuingia mikataba hii mibovu ni kama Dk Abdallah Kigoda mabaye ni marehemu yeye alifuta asilimia 15% yote ya mapato ya serikali iliykuwa ikipata kutokana na shughuli hiyo kwa kisingizio cha kamapuni ya Acacia kupata hasara kubwa ktk uchimbaji hu wa madini,viongozi wengine ni kama Nazir kalamagi aliyewahi kuwa waziri wa wizara hiyo,Sospeter Muhongo aliyewahi kuhudumu nafasi ya uwaziri mara mbili ktk wizara hiyo wakati wa wa rais Kikwete na Magufuli kisha kuondolewa kwa kujiuzulu baada ya kashfa zinazohusisha wizara hiyo na mikataba.

Taasisi na vitengo mbalimbali vinavyohusika ktk uchimbaji na machakato mazima wa madini pia vimehusishwa na kuingizwa ndani ya sakata hili baada ya kushutumiwa kuwa kwa makusudi baadhi ya maofisa na wagfanyakazi wa serikali walihujumu jitihada za serikali kwa kundekeza maslahi yao buinafsi na kuiweka nchi mahali pabaya.

Rais ameapa kulisimamia jambo hili na mengine yote yanayohusisha ubadhilifu wa mali za ummana kamwe hatishi na wanasiasa wala makampuni yanayotaka kumshitaki kwa kisingizio kuwa anavunja mkataba,yeye hatishi na ameagiza makontena yote aliyoyazuia kamwe yasitoke mpaka pale Acacia watakapokaa na kukubaliana kulipa pesa zote wanazodaiwa na serikali,kujisajili brella na kuanza mchakato upya.

Amesisitiza kuwa kuna umhumu wa kujengwa kwa matambo wa kuyeyusha madini hayo hapa nchini badala ya kusafirishwa kwenda nje na kuleta mianya ya wizi kwa walaji.

Serikali inaidai zaidi ya Trilioni 108 kamapuni ya Acacia kama kodi walizokimbia kwa miaka kadhaa ktk madini ya dhahabu pekee ambayo ni zaidi ya tani 1240.


 Rais amesema mikataba hiyo yote itarudishwa bungeni kwa ajili ya kuijadili upya na kumuagiza spia wa Bunge Job Ndugai kusimamia kwa uimara na kuwaondoa wale wote watakaokuwa wanaropoka hovyo bungeni na yeye atawashughulikia kikamilifu endapo wataropoka wakiwa nje.


Share :

Facebook Twitter Google+
0 Comments "RIPOTI YA PILI YA MAKINIKIA:WALIO HUDUMU WIZARA YA NISHATI NA MADINI KUANZIA 1998 KUKIONA"

Back To Top