BIASHARA YA MCHANGA YATISHIA UHAI WA VIUMBE DUNIANI

Mchanga ni miongoni mwa biadhaa muhimu na adimu na inayohitajika sana ulimwenguni kwasasa,mchanga una kazi kubwa ya kutumika ktk ujenzi wa majengo mbalimbali duniani,kuna aina nyingi za mchanga kulingana na mahali unapopatikana ktk uso huu wa dunia.

Kuna mcanga unaopatikana ndani ya na  pembezoni mwa mwambao wa bahari wenyewe uwa na kiwango kikubwa cha chumvi hivyo kuufanya kuwa sio bora zaidi ktk ujenzi,uko mchanga uanopatikana ktk mito,maziwa,jangwani .

Kwasasa ktk dunia mchanga sasa umekuwa bidhaa adumu sana na inayohitajika kwa kutumia njia yeyote ile,biashara hii imekuwa ikikuwa siku hadi siku hasa ktk miji mikubwa duniani ambapo kiwango cha ujenzi wa majengo marefu uko kwa kasi ya hali yajuu.

Kingo za mito na pembezoni mwa bahari zimeharibiwa kwa kiasi kikubwa ktk dunia kutokana na uchimbaji huu wa mchnga.

Nchi kama za Singpore,Indonesia,Umoja wa falme za kiarabu na baadhi ya nchi ambazo zina uhaba wa ardhi wamejikuta wakihitaji badhaa hii kwa kiwango kikubwa kwa ajili ya kuongeza eneo la arhi kwa ajili ya kujenga hoteli,viwanda,shule.

Duabai,Qatar,Singapore na Indonesia ni miongoni mwa nchi zinazolaumiwsa kwa kuhusika na baishara hii ya michanga,Biashara hii kwasasa inayoonekana kuwa na faida kubwa sana imekuwa ikimilikiwa na makampuni makubwa yanayoongozwa na magenge yenye nguvu ya kimafia.

Sehemu kubwa ya mwambao ya bahari imeharibiwa kwa kiasi kikubwa sana na kusababisha uharibifu wa kimazingira,mmomonyoko wa udongo,maisha ya viumbe hai wanoishi ktk maji,kuharibika kwa maeneo ya kilimo.

Wataalam wa mambo yasayansi ya maisha ya dunia wametaja kuwa uchimbaji wa mchanga unaondelea kwa kasi umeleta madhara makubwa kwa dunia na viumbe wake waishio,Uchimbaji huu umesababisha kuaharibu kwa mfumo wa maisha ya dunia ktk utafutaji wa chakula na uhai wao (Ecology or balance of nature) Ikolojia ni miongoni mwa njia kuu za maisha ya viumbe hai na mazingira ktk kutegemeana ili kuendeleza maisha.

Kitu kimoja cha msingi ktk dunia kinapoondoshwa au kupotezwa ktk eneo lake la asili uleta madahara makubwa kwa eneo na viumbe waishio sehemu hiyo.

Ujenzi wa madaraja,maghorofa na majengo mengineyo utumia badhaa hii adimu ya mchanga ambayo uchanganywa na Saruji.

Kwasasa baadhi ya nchi zimeachana nmatumiazi ya mchanga kama rasilimali ghafi ya ujenzi na kuelekeza machoyao ktk utumiaji wa Chuma na mbao (Steel,iron and Hard wood) ktk ujenzi wa majengo mbalimbali.






Share :

Facebook Twitter Google+
0 Comments "BIASHARA YA MCHANGA YATISHIA UHAI WA VIUMBE DUNIANI"

Back To Top