KIJUE KITU KIGUMU ZAIDI CHA ASILI KULIKO VYOTE KTK DUNIA!!

Kuna vitu vingi sana ulimwenguni au ktk sayari yetu hii ya dunia ambavyo vyengine ni vya kiasili na vyenginevyo ni vya kuundwa na wanadamu wenyewe,ktk kila sayari kuna aina mbalimbali za madini au vitu ambavyo vinapatikana ktkn sayari hizo.

Wataalam wa mambo ya miamba wamekubaliana kuwa ALMASI (DIAMOND) ndio kitu kigumu zaidi cha kiasili kuwahi kuwepo ktk sayari yetu hii ya dunia Aina hii ya madini sio ngeni miongoni mwa watu wengi hasa kwa kuisikia ukilinganisha na kuona au kuitambua,madini kama dhahabu,Tanzanite na mengineyo yamekuwa maarufu ulimwenguni kote kutokana na thamani yake ya kifendha pia na uadimu wake ktk kupataikana ktk dunia,

Sio sehemu zote unaweza kukutana na madini haya bali sehemu chache sana,almasi imekuwa ikitumika kwa kazi kubwa ya kuwa kama mapambo ktk vitu mbalimbali kama urembo wa mkufu,hereni,pete lakini pia imekuwa ikitumika ktk kuweka urembo ktk saa,gari,simu na vyengeinevyo ili kuonyesha thamani ya kitu hiko,pia utumika ktk kukatia vioo.

Almasi imeundwa kiasili kama madini kutoka ktk kitovu cha dunia (Mantle and Core) kwa mamilioni ya miaka na kuja taratibu kuelekea ktk uso wa ardhi.

Madini haya ya almasi ndio kitu kigumu zaidi ktk uso wa dunia kutokana na aina ya uundwaji na magandamizo mkubwa uliotumika.

Almasi inapatikana ktk nchi za Afrika kusini ktk majimbo ya Witwatersland,Transvaal toka kugundulika kwake miaka ya 1800s,Namibia,Tanzania (Mwadui shinyanga),Congo DRC,Botswana na maeneo mengine ulimwenguni.

PLATINUM na TITANIUM pia yanatajwa kuwa ni miongoni mwa vitu vigumu kuwepo ulimwenguni baada ya almasi.

Madini haya yote yanapatikana sehemu za chini sana za ardhi hivyo kufanya kuwa kazi ngumu,hatari na ya kutumia gharama kubwa ktk kuayatafuta na kuyaandaa ili kutumika ktk mambo mbalimbali.




 Platinium


Titanium

Share :

Facebook Twitter Google+
0 Comments "KIJUE KITU KIGUMU ZAIDI CHA ASILI KULIKO VYOTE KTK DUNIA!!"

Back To Top