JE WAJUA KWANINI TAIRI (MAGURUDUMU) ZOTE ZINA RANGI NYEUSI! JE KUNA TAIRI ZENYE RANGI TOFAUTI NA NYEUPE?

Matairi au magurudumu ni miongoni mwa vifaa muhimu sana ktk vyombo vya usafiri kama baiskeli,pikipiki,gari,ndege na aina mbalimbali za mitambo au mashine nyingi ili kuweka urahisi zaidi ktk kutenda kazi.
Ziko aina nyingi za magurudumu au matairi yanayotokana na chuma.mpira au hata mbao kuegemeana na aina ya chombo aua matumizi husika.

Kufikia sasa gari,ndege na mitambo mingi utumia matairi ya mpira tu ktk kuendeshea  mitambo na mashine hizo isipokuwa treni na mitambo mikubwa zaidi ambayo ina uzito mkubwa sana au kufanya kazi ngumu ktk mazingira magumu na mabazingira ya zaidi basi utumia magurudumu au nyororo za chuma ngumu ili kuweza kuhimili hali na uzito huo mkubwa zaidi.

Mnapo miaka ya 1900s Gurudumu la kwanza litokalo na malighafi ya mpira lilitengenezwa na kuwa na umbile la mduara huku likiwa na rangi nyeupe kabisa,Jua kwa magaurudumu ya mpira ni yenye uzito hafifu na ujazwa hewa nyingi ndani yake hivyo kufanya kile kilichobebwa kuwa chepesi zaidi ukilinganisha na aina nyingi za matairi kama ya chuma.

Tairi nyingi mpaka leo duniani zinatengenezwa kwa kutumia malighafi ya mpira (Rubber) na huwa zinawekewa Carbon ili kuzifanya kuwa nyeusi na imara zaidi wakati inapokuwa inatumika ktk barabara za lami au chini ambapo ukutana na ardhi ngumu na joto kali sana.

Joto kali litokalo na msuguano wa lami na mwendo kasi ukiongeza na jua kali hasa ktk nchi za kiafrika na asia ambazo kiwango cha jua uwa ni kikali zaidi.

Utafiti unaonyesha kuwa tairi za rangi nyeupe au rangi tofauti haziwezi kuvumilia mazingira magumu ukilinganisha na tairi zenye rangi nyeusi.

Tairi moja ya ndege kubwa kabisa iliyojazwa upepo au hewa kiasi cha 320 Psi ina uwezo wa kubeba tani 38,tairi hizi zinatakiwa kubadilishwa baada ya kutua au safari 500 ardhini,ndege kubwa uwa na tairi kuanzia 14-32 ambapo tairi moja ugharimu zaidi ya dola3,300 ambayo ni sawa na milioni laki mbili na sitini elfu 7,260,000.

Tairi kubwa zaidi za mitambo utengenezwa na kiwanda cha Bridgestone,Michelin na Goodyear vilivyopo chini ya kampuni kubwa ya Lego nchini marekani,tairi hizi za 59/80R63V-Vsteel E-lugs ambayo moja ugharimu zaidi ya dola za kimarekani 42,500 sawa na milioni tisini na tatu na laki tano 93500000 za kitanzania kwa tairi moja,ikiwa utahitaji jozi ya tairi sita ni zaidi ya dola milioni 5.5 za kimarekani.

Tairi za mpira ambao kwa sehemu kubwa ya malighafi hii ulimwa na ulimwa barani afrika hasa ktk nchi za afrika magharibi kama liberia,senegal,sierra leone na nyinginezo ndio zimeonekana kuwa tairi bora na imara zaidi kwa usalama wa watu na chombo husika.













Share :

Facebook Twitter Google+
2 Comments "JE WAJUA KWANINI TAIRI (MAGURUDUMU) ZOTE ZINA RANGI NYEUSI! JE KUNA TAIRI ZENYE RANGI TOFAUTI NA NYEUPE?"

Kwanini tairi isutumike ya rangi ya njano ikatumika ya rangi nyeusi

Back To Top