UPUNGUFU WA RASILIMALI MAJI KULETA VITA AFRIKA,ASIA

Kama inavyofahamika na kila mmoja wetu kwa kujua moja au mbili kati ya faida za maji kwa mazingira,wanyama,wanadamu,mimea kwa jinsi yanovyoweza kuleta maendeleo ktk uchumi wa kilimo,ufugaji,viwanda na hata ktk matumizi ya majumbani kama kufulia,kupikia,kujisafishia miili,makazi.

Maji yana kazi nyingi na muhimu zaidi ktk dunia yetu kwani asilimia 71% ya uso wa dunia umezingukwa na maji yanaweza kuwa ya bahari,maziwa,mito,mabwawa,chemichemi yakiwa ktk hali ya chumvi au baridi,kuganda au kimiminika,isipokuwa asilimia 29% tu ya uso wa dunia ndio kuna nchi kavu yakiwemo mabara na visiwa.

Maji yanaoykusudiwa kuleta mitafaruku na hatimaye vita ni maji baridi ambayo sana upatikana ktk mito,maziwa,mabwawa na chemichemi ambayo yapo kwa asilimia 3% tu na yale ya maji chumvi yakichukua sehemu kubwa zaidi ya asilimia 97%.

Maji baridi kwa kiasi kikbwa ndio utumika ktk shughuli za kilimo,kunywa,kupikia,kufulia,kunyweshea wanyama na kazi mbali mbali ndiyo yanayo onekana adimu zaidi baada ya mabadiliko ya hali ya hewa kuendelea kujitokeza kwa kass kubwa kutokana na uharibifu wa mazingira,ukataji wa misitu,moshi wa sumu kutoka viwandani ambavyo vyote kwa pamoja vimekuwa ni sababu kuu za hali hii ya upotevu wa maji safi na salama kwa matumizi ya kibinadamu.

Nchi kama Somalia,mauritania,sudani,niger,iraq,uzibekstan,pakistan,misri,turkemenstan na syria ndizo nchi zilizo kwenye hatari zaidi kukubwa na janga hili la ukosefu wa maji safi kwa matumizi yao,maeneo mengi yalikuwa na hali ya kuganda barafu hasa kule arctic na antactica kuameanza kuonekana barafu zake zinayeyuka kwa kasi.

Nyanzo vingi vya maji safi ambavyo vilitegemewa sana na jamii vimepotea kwa kukauka ua kupungua kwa kasi kubwa,hali hii imepelekea migogoro ya kijamii na hata nchi kwa nchi kwa watu kushindwa kulima,kufuga na kufanya shughuli zinazotegemea maji kwa kiasi kikubwa.

Baadhi ya nchi ambazo zinatumia chanzo kimoja cha mto nile kama Uganda,ethiopia,sudani,chad,misri na nyenginezo zikiingia ktk migogoro mikubwa mara kwa mara ktk matumizi ya maji yatokanyo na mto huo mrefu zaidi barani afrika.






 Mimea,wanyama vyote kwa jumla vikionekana kufa na vyanzo vya maji kukauka baada ya mvua kutokunyesha kwa mda mrefu na kuwa na vipindi virefuzaidi vya jua kali.




Share :

Facebook Twitter Google+
0 Comments "UPUNGUFU WA RASILIMALI MAJI KULETA VITA AFRIKA,ASIA"

Back To Top