PAUL KAGAME AIKAMATA RWANDA KWA MARA YA TATU BAADA YA KUSHINDA UCAHAGUZI KWA KISHINDO

Paul Kagame ameshinda kwa kishindo kwa mara ya tatu ktk uchguzi mkuu uliofanyika juzi alhamisi na jana kutangazwa kama mshindi wa uchaguzi huo ulikuwa umepambwa na wagombea wa upinzani wawili.

Kagame anayeiongoza nch ya rwanda toka mwaka 1994 amekuwa akionekana kuwa ni kiongozi shupavu na mpenda maendeleo na wananchi walio wengi wa rwanda hasa kwa kuzuia machafuko ya kisiasa,kikabila na kuleta maendeleo ya haraka kwa kuweka nidhamu kubwa kwa serikali.

Zaidi ya wananchi milioni 5.4 ambao walikuwa ndio wapiga kura halali kwa uchaguzi huu,asilimia 98% ya wapiga kura hao wamepigia Paul Kagame.

Rwanda ni miongoni mwa nchi za afrika mashariki ambazo uchumi wake unakuwa kwa kasi zaidi licha ya nchi hiyo kuwa na ufinyu wa rasilimali kama ardhi,watu wamekuwa wakijitahidi sana kupiga hatua kwenye swala zima la kupeleka nchi yao mbele kimaendeleo.

Ktk jumuiya ya mataifa ya nje Kagame anaonekana kama mtu asiyejali demokrasia na utawala wa haki na sheria hasa kwa kutawala kwa mabavu,kufifisha vyama vya upinzani na harakati za mashirika yasiyo ya kiserikali kufanya kazi ndani ya nchi hiyo,pia Kagame amekuwa akibadili katiba na kujiongezea mda wa kutawala zaidi nchi hiyo ikiwa ni kinyume na matakwa ya umoja wa mataifa.



Share :

Facebook Twitter Google+
0 Comments "PAUL KAGAME AIKAMATA RWANDA KWA MARA YA TATU BAADA YA KUSHINDA UCAHAGUZI KWA KISHINDO"

Back To Top