HIZI NDIZO BIASHARA HARAMU ZENYE KUINGIZA MABILIONI YA DOLA NA KUWAPA WATU UTAJIRI MKUBWA

Tambua kuwa biashara haramu ndio kazi zenye kuingiza kiasi kikubwa sana cha fedha kwa mda mfupi zaidi.


Biashara haramu ni biashara zinazofanyika licha ya vyombo vya dola kupiga marufuku kutokana kiwango kikubwa cha madhara ya kiafya,mazingira,kijamii na kiuchumi.

Baadhi ya biashara hizi ni:-


1.Uuzaji wa madawa ya kulevya kama heroin,mandrax,opium,marijuana au bangi ambazo uingiza zaidi ya dola za kimarekani billion 300 kwa mwaka.










2.Ukahaba (umalaya) ni biashara ya kuuza mwili kama sehemu ya kustarehe,biashara hii imetapakaa ulimwenguni kote hasa sehemu za miji na majiji makubwa,kazi hii inaingiza zaidi ya pound bilioni 5.7 za uingereza.







Kazi hii imechangia kuenea kwa magonjwa kama ukimwi kwa kiwango kikubwa.

3.Utoroshaji na uuzaji wa wanadamu ( utumwa)-Hii ni miongoni mwa biashara kubwa duniani inayofanywa na makundi ya watu kwa kuwatorosha watu kwa kutaka au kwa lazima na kuwapeleka nchi za ulaya,Asia na amerika ktk kufanya kazi kama za ngono,uuzaji wa madawa,kazi za ndani kama watumwa.



Biashara hii uingiza zaidi ya dola bilioni 31.6 za kimarekani

4.Uuzaji wa viungo vya binadamu pia ni miongoni mwa biashara zinazokuwa kwa kasi kubwa na kuingia pesa nyingi sana,kazi hii ufanyika kwa lazima au kutaka kwa mtu,viungo kama figo,moyo,ini uchukuliwa na kwenda kupandikizwa kwa watu wengine walio na matatizo ya viungo hivyo.



Kazi hii uingiza dola bilioni 1 za kimarekani.

5.Uuzaji wa silaha wa kinyemela pia ni bishara kubwa duniani hasa ktk nchi zenye machafuko kama Afghanistan,Pakistan,Iraq,Syria,Palestine,Congo DRC n.k silaha uuzwa kwa makundi ya waasi.



Kazi hii uingiza zaidi ya dola bilioni 1 za kimarekani.

Zipo biashara nyingi sana haramu zinazofanywa na kuwapa utajiri mkubwa watu duniani tena kwa mda mfupi sana.

Ufanyaji wa biashara hizi ni hatari sana kwani ikitokea kukamatwa na vyombo vya dola hasa ktk nchi za kigeni kama China zinaweza kukugharimu uhai wako kwa kuhukumiwa kunyongwa au kifungo cha maisha ukiacholia mbali hatari za magonjwa na kupasuka kwa madawa yakiwa tumboni kunakoweza kukusababishia kifo.














Share :

Facebook Twitter Google+
0 Comments "HIZI NDIZO BIASHARA HARAMU ZENYE KUINGIZA MABILIONI YA DOLA NA KUWAPA WATU UTAJIRI MKUBWA"

Back To Top