KUBENEA ASEMA MWAKYEMBE ANA CHUKI BINAFSI NA MAGAZETI YAKE

Mwandishi wa habri saidi Kubenea anayefanyia kazi ktk magazeti ya Mawio na mwanahalisi amemlalamikia waziri wa habari,sanaa na michezo Harrison Mwakyembe kuwa hatua ya kulifungia Gezeti la mawio kwa kutoa taarifa na picha za maraisi waliopita Jakaya Mrisho kikwete na Benjamin wiliam Mkapa kwenye kurasa za mbele za gazeti hilo.

Kufungiwa kwa Gazeti hilo kwa kosa la Kuweka picha za Maraisi hao kunatokana na kashfa inayoendelea juu ya Makampuni,mikataba mibovu ya madini iliyoingiwa nyakati za utawala wa Marais hawa.

Kubenea alilalama zaidi na kusema mwakyembe na yeye hawana maelewana toka awali hasa ktk vyombo vyake vya habari toka kuandika kwa sakta la umeme wake wa upepo wa huko mkoani singida.

Gazeti hili ambalo lilishachapishwa toka jumatano ili litoke alhamisi ambapo lilishasambazwa ktk mikoa liligharimu zaidi ya shilingi milioni 20 limeingia ktk hasara kubwa,kubenea aliongea na radio ya kiswahili ya DW wao watamwandikia Rais Magufuli Barua juu ya kumuomba aliachie liendelee kutoa taarifa kwani vyombo vya habari havipangiwi nini cha kuandika,

Share :

Facebook Twitter Google+
0 Comments "KUBENEA ASEMA MWAKYEMBE ANA CHUKI BINAFSI NA MAGAZETI YAKE"

Back To Top