
Uwanja huu mkubwa wa kijeshi nchini umegharimu zaidi ya shilingi bilioni 137 na milioni 600 za kitanzania ktk ukarabati wake mkubwa zilizotolewa na serikali ya watu wa jamhuri ya china kwa serikali ya Tanzania.
Kambi hii ni miongoni mwa kambi kongwe nchini ilianzishwa mwaka 1970 huko morogoro na kuwa kambi muhimu kwa jeshi la anga nchini,Uzinduzi wa kambi hii ulifanyika siku moja tu baada ya Rais kutoka kumaliza ziara yake kwa mikoa ya pwani,lindi na mtwara .
Uwanja huu wa ndege ni miongoni vya viwanja vya ndege vikubwa vyenye uwezo wa kutua ndege kubwa ktk afrika mashariki.
Ktk uzinduzi huo uliohudhuriwa na maafisa wa juu wa jeshi ulipambwa na mkuu wa nchi kwa kushika bunduki yenye risasi za mpira na kupiga hewani kama ishira ya kijeshi ktk uzinduzi wake.
0 Comments "MAGUFULI AFUNGUA UWANJA WA NDEGE WA JESHI NGERENGERE"