MADEREVA NA UTINGO WA MALORI HATARINI KUKOSA AJIRA

Zaidi ya madereva na utingo wa magari makubwa ya kusafirisha mizigo kwenda mikoani na nchi za jirani kama Rwanda,uganda,DRC,zambia,malawi wako hatarini kukosa kazi zao kutokana na hali ya upatikanaji wa mizigo hasa ktk bandari ya Dar es salaam inayohudumia nchi zaidi ya sita.

Madereva na utingo hao wapatao zaidi ya 23000 wanakuwa hatarini baada ya malori 11500 kushindwa kuingia barabarani kwa kukosa bidhaa za kusafirisha kwenda maeneo mbalimbali,kuna malori zaidi ya 21000 yaliyo sajiliwa kufanya kazi hiyo.

Licha ya kuboreshwa kwa utendaji kazi na miundombinu ya bandari hiyo ya Dar es salaam hasa ktk kipindi hiki cha awamu ya tano kwa kupunguza vipingamizi vya jinsi ys kutoa mizigo ndani ya bdandari hiyo vilivyokuwa vimeambatana na ufisadi,rushwa na uzembe ktk utendaji kazi bado hali inaonekana kuwa tete.

Hadi kufikia mwaka 2015 mwishoni malori mengi yalikuwa barabarani kiasi cha kuleta msongamano wa magari ndani na nje ya jiji ya dar es salaam na kupewa ratiba  ya kuingia ndani ya jiji hilo,serikali ilizungumza kuwa ujenzi na uboreshaji wa reli unahitajika ili kupunguza msongamano wa magari,uharibifu wa barabara,mlundikano wa mizigo bandarini.

Kulikuwa na ukwepaji mkubwa wa kodi za serikali kwa mizigo ya wafanyabiashara wengi na kufanya kuingiza mizigo kwa kiasi kikubwa kwa kupitia njia za panya.

Share :

Facebook Twitter Google+
0 Comments "MADEREVA NA UTINGO WA MALORI HATARINI KUKOSA AJIRA"

Back To Top