GENERALI WA POLISI ALIYEUAWA UGANDA AZIKWA

Ijumaa ya tarehe 17/3/2017 watu wenye bunduki walivamia gari ya Inspekta msaidizi wa jeshi la polisi ya nchini Uganda Bwana Andrew Felix Kaweesi,dereva na mlinzi wakewakiwa ktk mazingira ya nyumbani kwa ispecta generali msaidizi.

Watu hao walikuwa wakijihami kwa silaha za moto walimuua Bw.Kaweesi na wenzie papo hapo kwa kuwapiga risasi za hivyo mwilini na kutoweka ktk mazingira ya kutatanisha.

Mpaka sasa sababu ya kuuwawa kwao haijajulikana ila watu walihisiwa kuhusika na mauaji hayo wamekamatwa na kuanza kuhojiwa na jeshi la polisi.

Mauaji hayo yalimstua sana Rais wa Uganda Bw.Yoweri Kaguta Museveni na kuyalaani na kusema ni vyema sana sehemu zote zenye misongamano ya watu,makutano ya barabara zote ni muhimu kuweka kamera maalum za usalama ili kujua kutunza watendaji wa matukio kama hayo ya mauaji na uhalifu ili kusaidi polisi na vyombo vya usalama ktk kutafuta ushahidi na wahusika.

Inspekta huyu amekuwa wa kwanza kufa ktk polisi 70 wa kiume na 12 wa kike waliohitimu mafunzo yao mwaka 2001.

Felix Kaweesi amezikwa leo na kupata heshima zote za jeshi la polisi.



Share :

Facebook Twitter Google+
0 Comments "GENERALI WA POLISI ALIYEUAWA UGANDA AZIKWA"

Back To Top