TETEMEKO LA ARDHI ZIWA TANGANYIKA

Imeripotiwa  kutokea kwa tetemeko la ardhi kwa sehemu zote zinazo zunguka ziwa tanganyika ikiwemo kigoma na nchi za jirani kam Congo DRC,Zambia,burundi na mikoa ya karibuni na ziwa hilo,Tetemeko hilo lenye ukubwa wa Ritcher scale 5.7 limepiga hasa ndani ya ziwa tanganyika ambalo limepitiwa na bonde la ufa la afrika mashariki lilianzia nchini jodan.

Ziwa Tanganyika ndio ziwa lenye kina kirefu kuliko maziwa yote duniani linalopatikana nchini Tanzania,burundi,na Congo hivyo Tetemeko hilo limeasili maeneo hayo japo hakuna kifo wala uharibifu wa mali za watu uliolipotiwa.

Tetemeko limepiga maeneo ya nchi jirani ya Zambia ktk mji wa Kaputa uliopo kilometa 47 kutoka ziwa Tanagnyika lilipo,asili au kitovu cha kilometa kumi 10 kutoka chini ya ardhi,majira ya saa kumi na mbili asubuhi(6:32) leo ijumaa.

Si mara y kwanza kwa tetemeko kutokea ktk ziwa hili kwani mwaka 2005 tetemeko lenye vipimo vya Ritcher scale 6.8 na kuafanya uharibifu,lakini mwaka jana lilitokea mkoa wa kegera na kuathiri maeneo mengi ya mkoa huo kama kuanguka kwa majengo na vifo.

Share :

Facebook Twitter Google+
0 Comments "TETEMEKO LA ARDHI ZIWA TANGANYIKA"

Back To Top