AFRIKA YA KUSINI NAO WAJA JUU DHIDI YA WAHAMIAJI

Wananchi wa afrika ya kusini wameamua kuingia barabarani kwa Mara ya pili kupinga uwepo wa wahamaji Wengi wanaozidi kufulika nchini humo kutoka mataifa ya mbali na jirani.

Ikumbukwe hii ni Mara ya pili  kwa waafrika kusini kufanya matukio haya ya kuandamana juu ya kupinga uingiaji na uwepo wa wageni ndani ya nchi yao,miaka michache nyuma waliandamana na kuwapiga vibaya wahamiaji kutoka Zimbabwe waliokimbia hali  ngumu ya uchumi iliyotokana na mfumuko wa bei na kwenda nchini humo kwa ajili ya kutafuta kazi.

Maandamano hayo yanakuja baada ya malalamiko kutoka kwa wananchi juu ya kukosekana kwa ajira miongoni mwa wazawa wa nchi hiyo inayotokana na ujio mkubwa wa wahamiaji kutok mataifa wa afrika.

Waandamanaji walionekana wakishika silaha kam mapanga,shoka,nyundo na magongo wakiashiria kutaka kuwapiga wahamiaji.

Rais  wa afrika kusini Jacob Zuma amewasihi raia  zake juu ya kuwa watulivu na kutunza amani ya taifa lao.


Share :

Facebook Twitter Google+
0 Comments "AFRIKA YA KUSINI NAO WAJA JUU DHIDI YA WAHAMIAJI"

Back To Top