Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Dr.john pombe Joseph magufuli amemuapisha Mkuu wa majeshi mpya leo ikulu mapema.
Mkuu huyo wa majeshi anaejulikana kama Venance S.mabeyo alietuliwa wiki iliyopita ktk sherehe za wiki ya mahakama ambapo mgeni rasmi alikua raisi magufuli.
Pia raisi magufuli amemuapisha Mkuu na mnadhimu wa chuo cha ulinzi cha jeshi ndugu aloyce mwakibolwa.
Nafasi ya Mkuu wa majeshi iliachwa wazi na Mkuu wa zamani Davis mwamunyange.
Dk magufuli amezungumzia sakata swala la madawa ya kulevya linalotokota wiki hizi,kuwa kashfa hizo hazina umaarufu wa ukubwa,vyeo au ukaribu wa mtu yeyote ataketuhumiwa akamatwe na sheria ifuate mkondo wake hata kama atakuwa mke wake(Janeth) akamatwe tu.
Aidha alimwambia IGP Ernest mangu kuwa anajua alipigiwa simu na watu kuwa apunguze nguvu kutaja wahalifu Ila hakuwasikiliza kabisa na endapo angefanya huvyo basi leo cheo kile asingekuwa nacho tena.
Mkuu wa mkoa Dar es salaam amepongezwa kwa bidiii na jitihada anazozionyesha juu ya swala hilo,lakini pia ameongeza kuwa hakufanya uteuzi wa Mkuu mpya wa majeshi kwa kuhofia kuona watu wangehisi amemtumbua Davis mwamunyange.
Sherehe hizo zimehudhuriwa na raisi wa Zanzibar dk Mohamed shein,waziri mkuu majaliwa kassim majaliwa.
Related Post:
- KUTANA NA MATOKEO YA KIDATO CHA SITA NA YALE YA VYUO VYA UALIMU 2017
- UJENZI WA BARABARA YA MTWARA,TANDAHIMBA,NEWALA WAPAMBA MOTO
- RAIS MAGUFULI AZINDUA BARABARA YA LAMI KALIUA-KAZILAMBWA TABORA
- ASKOFU GWAJIMA ALIAMSHA DUDE KWA KUONYESHA JEURI YA FEDHA BAADA YA KUNUNUA NDEGE YAKE BINAFSI
- ALIYEKUWA WAZIRI WA MADINI WILLIAM NGELEJA AREJESHA PESA ZA ESCROW SERIKALINI
0 Comments "RAIS MAGUFULI AMUAPISHA MKUU WA MAJESHI MPYA"