MIAKA 40 YA UTAWALA WA CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM)

Kila ifikapo tarehe 5/2 kila mwaka chama cha mapinduzi usheherekea kumbukumbu ya kuundwa na kuzaliwa cha cha mapinduzi 5/2/1977 kilichozaliwa kwa muunganiko wa vyama vya ASP cha zanzibar na TANU cha tanganyika vilivyokuwa vinatawala kwa kipindi hiko.

Viongozi walioshiriki ktk muungano huo mwalim julius kambarage nyerere na hayati shekh abeid amani karume kwa upande wa zanzibar,walifanya muungano huo ili kuunda chama kimoja tu kitakachotawala sehemu zote mbili,kabla ya hapo  tarehe 26/4/1964 kulifanyika muungano wa nchi hizi mbili yaani Tanganyika na zanzibar na kuzaliwa TANZANIA.

Kwa upande wa tanganyika mpaka sasa wametawala maraisi watano yaani hayati Mwalimu j.k nyerere toka uhuru hadi 1985, ally hassan mwinyi hadi 1995,benjamin william mkapa hadi 2005,jakaya mrisho kikwete hadi 2015 na sasa yupo ndugu john pombe joseph magufuli ambae ameshika madaraka kwa tiketi ya ccm toka 5/11/2015.

Ccm imejipanga na kuanza kubadili mfumo wa utawala wa chama na uongozi wa serikali na kushughulikia matatizo ya jamii zaidi ikewemo afya,miundombimu,rushwa,vyeti feki,wafanyakazi hewa,kukusanya mapato zaidi,kutumia vyanzo vya pesa vya ndani zaidi na sio misaada,kujengan viwanda vingi,kuongeza ajira,kupunguza matumizi yasio ya lazima kwa wafanyakazi wa serikali,kupunguza makato ya kodi ktk mishahara,kutoa mikopo zaidi kwa wanafunzi wa vyuo,kutoa elimu ya msingi hadi kidato cha nne bure,kuwajibubika sehemu za kazi,kupunguza mishahara mikubwa kufikia milioni 15 kwa mwezi,kupunguza safari za serikali za nje n.k.

uchaguzi wa mwaka 2015ulikuwa uchaguzi wenye hamasa kubwa kwa kile kilichoonekana kuhama na kujiudhulu kwa wanachama wakubwa ktk vyama,idadi kubwa ya wapiga kura kujitokeza vituoni.




Share :

Facebook Twitter Google+
0 Comments "MIAKA 40 YA UTAWALA WA CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM)"

Back To Top