Majira ya saa mbili kasorobo (1:45) asubuhi hii ya jumanne 31/1/2017 eneo la mtwara Mjini manispaa ya mtwara mikindani mkoani mtwara mvua kubwa inayoambatana na ngurumo,radi na pepo kali inayesha na kusababisha usumbufu kwa wakazi wa eneo hilo has a wanafunzi na wafanyabiashara wa Mjini hapa.
Zaidi ni ujenzi wa uboreshaji wa miundombinu ya barabara nyingi za hapa Mjini pamoja na ujenzi wa mifereji au mitalo ya kupitisha maji ya mvua kuwa bado mingi haijakamilika hivyo kuhofiwa kwa kuondolewa kwa vifusi na dhana za ujenzi ambazo ziko maeneo ya ujenzi.
Pia kuna hofu ya kuweza kutokea mlundikano wa maji ktk mitalo hiyo na hats makazi ya watu endapo mvua hiyo itaendelea kunyesha kwa kasi hiyo.
Kumekuwa na kukosekana na kususuasua kwa unyeshaji wa mvua mkoani mtwara ambapo zilitarajiwa kuanza toka mwezi desemba.
0 Comments "MVUA KUBWA INAYOAMBATANA NA PEPO,NGURUMO KALI INAENDELEA KUNYESHA MTWARA"