WALIMU 21,780 WALIOFELI MITIHANI SHULE ZA MSINGI KUTIMULIWA KAZI

Zaidi ya walimu 21,780 kutoka jimbo la Kaduna lililopo kaskazini mwa nigeria wako kilioni baada ya zoezi la ajabu na kustukiza kufanyika kwao kwa kupimwa kwa kuijibu mitihani ya wanafunzi wa shule za msingi  na hatima yake kuambiwa waifanye wao.

Majibu ya mitihani hiyo yalionekana mabaya kabisa kwa upande wa walimu baada ya kusahihishwa,hali hii ilimsitua gavana wa jimbo hilo la Kaduna Ndugu Nasri-el Rufai na kutoa maamuzi magumu ya kutaka kuwafukuza kazi walimu wote waliofanya jaribio hilo na kufeli.

Gavana Rufai amenukuliwa akisema kuwa kwa sasa wako mbioni kuajili walimu wapya wenye vigezo na uwezo zaidi na kuwaondoa wale wote waliofanya vibaya.

Ikumbukwe kuwa Kaskazini mwa Nigeria ndio kwenye majimbo masikini zaidi ktk nchi hiyo,Kuanzia miundombinu ya Elimu,afya si hivo tu majimbo  haya ndio majimbo yanayokumbwa na machafuko ya vita za wenyewe kwa wenyewe zinasosababishwa na ubaguzi wa kidini,kikabila na kisiasa.

Makundi kama Boko Haram ndio makundi yanayosumbua kaskazini na nchi nzima ya nigeria  kwa kufanya mashambulizi ya kujitolea mhanga,shule nyingi za msingi na sekondari zimeharibiwa vibaya au kuchomwa moto na vikundi hivi na kusababisha kufungwa kwa shule hizo hadi sasa na zaidi ya wasichana 300 walitekwa nyara na kikundi hiko na wengi wao hawajapaikana hadi leo.



Kiwango cha elimu kwa nigeria kaskazini kimekuwa cha chini zaidi ukilinganisha na kusini mwa nchi hiyo,hali hii imefanya walimu wengi kuacha au kukimbia kazi ktk maeneo hayo kwa kuhofia usalama wa maisha yao.

Share :

Facebook Twitter Google+
0 Comments "WALIMU 21,780 WALIOFELI MITIHANI SHULE ZA MSINGI KUTIMULIWA KAZI"

Back To Top