TAJARI MKUBWA AFANYA MAUAJI LAS VEGAS HADHARANI

Stephen Paddock mwenye umri wa miaka 64 akiwa ni miongoni mwa matajiri wakubwa nchini marekani ameushangaza umma wa wamarekani baada ya kuvamia Ukumbi wa Hotel Las Vegas kulikokuwa kunafanyika tamasha la muziki la kila mwaka lijulikanalo kama Route 91 Festival na kufyatua risasi kwa watazamaji walikuwemo ktk ukumbi huo na kuua zaidi ya watu 59 ambapo 20 walikufa papo hapo na wengine kufia hospuitalini baada ya mda mchache wa tukio hilo.

Zaidi ya watu 500 wamejeruhiwa ktk tukio hilo baya kabisa na kutisha kuwahi kutokea ktk visa vya aina hii nchini marekani,Stephen alituia bunduki ya nzito ya matumizi ya kijeshi ya risasi za rasha rasha ambayo mara nyingi hutumika ktk medani za vita na si kwa ajili ya kujilinda,polisi wameshangazwa sana na tukio hilo pia na umiliki wa aina hiyo ya silaha ya kijeshi na tajiri huyo.

Upekuzi umeonesha kuwa nyumbani mwa bwana huyo kumekutwa na silaha za aina hiyo zaidi ya 18 na vilipuzi vya iana nyingi ambavyo walihisi vilikuwa vikitaarishwa kwa ajili ya uhalifu zaidi,polisi wameshindwa kifahamu sababu za msingi kwanini tajiri huyu amefikia uamuzi huo wa kuua watu wengi kiasi hiki hasa ktk jimbo hili la Nevada ktk mji wa Las Vegas ambao ndio mji wa starehe zaidi nchini marekani,mji huu una sehemu nyingi za starehe kama mahoteli ya nyota tano,kumbi za za miziki kubwa na migahawa ambapo watu matajiri,maarufu na wapenda starehe wengi ufika ktk eneo hili kwa ajili ya kuburudika.

Stephen aljiua yeye mwenyewe mda mchache sana baada ya tukio hilo,visa hivi ni vingi kutokea nchini marekani kwa watu kuamua kuvamia kumbi,mikusanyikon na vyuo na shule kisha kuua watu kwa kuwamiminia risasi watu hovyo,wamarekani ni watu wanao ruhusiwa kununua na kumiliki silaha kama bunduki ndogo kwa ajili ya usalama wake binafsi,hii ni miongoni mwa sababu ya kuongezeka kwa visa hivi.





Share :

Facebook Twitter Google+
0 Comments "TAJARI MKUBWA AFANYA MAUAJI LAS VEGAS HADHARANI"

Back To Top