ZIJUE NJIA CHACHE ZA KUMSHIKA (KUMKAMATA) MKE,MUME AU MCHUMBA ALIYEANZA USALITI KTK MAHUSIANO!!!

Unapozungumzia mahusiano ya kimapenzi yawe ktk ndoa au nje ya ndoa bila shaka unakuwa umegusa changamoto lukuki ambazo wawili hawa wanaweza kukutana nazo  ambazo kwazo ndizo zinazoweza kufanya mahusiano yao kuimarika,kudumu zaidi na kutimiza lengo la  kuanzisha mahusiano yao au kuweza kukatisha safari hiyo nyakati yeyote.



Ziko changamoto nyingi ambazo wawili wakikutana nazo  zinaweza kuwafanya kuingia ktk migogoro ya kimahusiano na hatimaye kuaharibu mahusiano yao na kubaki kuwa historia tu.

Asilimia kubwa ya vikwazo hivi vya kimahusiano vinavyosababisha kuharibika,kutokuwa na maelewano na hata kuvunjika kwa ndoa au mahusiano hayo utakana na mabadiliko ya kitabia za wahusika.




Licha ya kuwepo vitu kama kushuka au kupanda kiuchumi,makundi ya kirafiki,mabadiliko ktk mwili yatokanayo na ajali,magonjwa makubwa,kuchonganishwa na     watu n.k.

Leo nitazungumzia tabia  moja sugu na kubwa na inayohusika kuleta mogogoro,kutoelewana na hata kusambaratisha mahusiano aua ndoa hiyo na mwishowe  kuweka familia na jamii ktk mazingira magumu ya kimakuzi,kimaisha.



Tabia hii ni ile ya (USALITI,KUCHEPUKA KTK MAHUSIANO) Ambayo inahusika ktk uvunjaji wa mahusiano na ndoa za watu kwa zaidi ya asilimia 70%.

Kwanza kabisa nitaanza na baadhi ya sababu zinazoweza kusababisha mmoja ktk ya wapenzi au wanandoa kufanya usaliti huo:-

1-Kutoridhishwa ktk kitendo cha ndoa au ngono tofauti na awali kunakotokana na udhaifu wa mtu  husika au magonjwa.



2-Tamaa ya kupata uhueni ya maisha kutoka kwa mtu  mwingine baada ya kuona mweza wake hali yake si nzuri.

3-Kutokuwepo na maadili ya kidini  kwa husika.

4-Kuchangamana aua kuiga marafiki zako wa karibu ambao wao wanayafanya hayo kwa kuwa ni mambo ya kawaida hivyo kushawishika au kukushawishi kufanya hivyo.


5-Kupungua kwa mihemko kwa mpenzi wako wa awali hivyo kukulazimu kusaka  penzi  jipya.

6-Wengine usaliti au kuchepuka kwa ajili ya kutaka kulipiza kisasi  kwa Yale anayotendewa na mwenza wake,hivyo ufanya ili kuifariji nafsi kuwa amelipiza.



7-Kushindwa kupata alichokusudia kutoka kwa mpenzi wa awali au kutafuta ujuzi mpya.

8-Kuingia ktk matumizi ya pombe na vilevi vya madawa ya kulevya kupindukia.

9-Kuongezeka kwa manyanyaso,malumbano au mapigano ya Mara kwa Mara.

10-Kushindwa kutimiza wajibu wako wa huduma aua kujituma ndani ya ndoa ukiwa majukumu ya ndoa,chakula usafi wa nyumbani,mazingira na hata mwili wako.



ZIFUATAZO NI NJIA CHACHE ZITAKAZOKUWEZESHA KUMJUA MPENZI AU MWANDOA MWENZIO ANAYEKUSALITI AU KUCHEPUKA:-


Kwa nyakati tulizonazo kwa sasa za maendeleo ya  sayansi na teknolojia njia ya mawasiliano ndio nyepesi inayokuwezesha kumtambua mwenzio kuwa ameanza au anafanya uchepukaji.

Matumizi ya simu,kompyuta,tablets ktk mitandao ya kijamii kama Facebook,WhatsApp,Twiter,badoo,e mail,mesegi,simu kupiga simu zimekuwa zikichangia kwa kiasi kikubwa ktk kuvunja ndoa na mahusiano ktk jamii.

Dalili au mabadiliko yafutayo yatakufanya kugundua usaliti wa mwenza wako!

1-Kuzidi kwa matumizi ya simu,kama mesegi,kupigiwa simu na kupokea au kujibu simu hizo kwa usiri mkubwa.


Wakati Fulani utoka mbali na ulipo wewe,kupunguza sauti ya Siku ya kuongelea,kupitia na hata kufuta historia ya mesegi na simu ziingiazo na kutoka.

2-Kutokutaka kuguswa,kupokewa kwa simu yake na mtu yeyote yule,kuizima anapokuwa jirani nawe kuepuka kupigiwa au kutumia jumbe,na endapo utadiliki kufanya hivyo unaweza kuleta ugomvi mkubwa sana.



3-Kuwa na idadi kubwa ya marafiki na kupenda kutumia mda wake mwingi zaidi kuwa na hao marafiki kuliko kuwa na wewe.

4-Kubadilika kitabia ktk utendaji wa mambo yake kama kuoga Mara kwa Mara kila anaporudi kutoka safari zake,kubadilika harufu ya jasho lake aua kuwa na haruyu ng'eni kaa ya pafyumu,sigara,pombe na salama ndogo ndogo ambazo siziso za kawaida.

5-Kuvaa na kupendeza huku akitumia mda mwingi zaidi ktk kujipendezesha pindi anapotaka kutoka safari zake za nje,wakati Fulani kuvaa kinyume na mazoea yake.



6-Kuwa makali sana pindi unapojaribu kuhoji baadhi ya mambo yanayoonekana kuhusa mambo yake hayo ya nje hata ukiwa unahisi tu.

7-Kuomba au kuwa na safari na mitoko ya ghafla isiyo na ratiba Maalum na hata ukijaribu kukataza au kutoa ushauri kuwa atakwenda Siku nyingine uonekana kuyokulewa na unaweza kuzua mtafaruku mkubwa hivyo kulazimisha kwenda safari hiyo na mbaya zaidi uchelewa kurudi.



8-Kushindwa kukutazama pindi unapohoji juu ya Tabia zake na kuanzia kwa tabia ng'eni kama za matumizi ya sigara,pombe ghafla.

9-Kupungua kwa hamu au kugoma kabisa kutenda tendo la  ndoa kwa kusingizia kuumwa,kuchoka Mara kwa mara,hii utokana na kumaliza haja zake za kingono nje zaidi.



10-Kuongezeka kwa malumbano kushuka kwa kiwango cha heshima,adamu na usiri wa hali ya juu ndani ya maisha ya mwenza wako ikiwemo na kuongezeka kwa dharau ndani ya mahusiano.



Zipo sababu nyingi San zinazowezesha kujua mabadiliko ya usaliti au uchepukaji wa mwenza wako Ila kikubwa zaidi inahitaji umakini wa hali ya juu ktk kufuatali Tabia hizo kwa kipindi kirefu kwa kina mpaka pale utakaporijidhisha au kuweka mitego na kunasa ushahidi wa wazi ili kufanya maamuzi kwani mwenza wako anaweza kuonyesha au kuwa na baadhi ya Tabia tulizotaja hapo juu Ila ikawa hana Tabia ya usaliti wa kuchepuka.



ZINGATIA:-
Tabia hizi za usaliti na uchepukaji ktk mahusiano zinawezwa kusabanishwa  na moja ya mwanandoa au mwanamahusiano kutokana na kushindwa kusoma na kwa kina ktk tabia na matakwa ya nafsi,hivyo ni muhimu sana kujuana kwa kitabia kwa kina ili kuepuka matatizo haya.



Pia jua wazi mahusiano ni yana Pande sawa za shilingi hayuko aliye zaidi kuliko mwenziwe hivyo mnapaswa kuwa wanyenyekevu,kuhurumiana,kuthaminiana,kupendana na kufanyiana wema kila Siku ili kuboresha mahusiano yenu na kuondoa roho aua mawazo ya kufanya mmoja wenu kuanza  kuwaza kuchepuka  au usaliti.



Utakuwa shahidi wapenzi au ndoa iliyo ktk kiwango cha juu sio la kwa kutongonzwa kirahisi ukilinganisha na mahusiano na ndoa zilizopo ktk migogoro.

Hii ni kwa sababu nafsi ya mwanadamu imeumbwa kupenda zaidi sehemu inayomfanyia mambo mema na kuchukia inapofanyiwa maovu na manyanyaso.








Share :

Facebook Twitter Google+
0 Comments "ZIJUE NJIA CHACHE ZA KUMSHIKA (KUMKAMATA) MKE,MUME AU MCHUMBA ALIYEANZA USALITI KTK MAHUSIANO!!!"

Back To Top