WAISLAM KUSHEHEREKEA SIKUKUU YA IDD EL FITRI JUMATATU

Kutokana na kutoonekana kwa mwezi siku ya leo jumamosi juni 24 2017 ambapo waislamu walikuwa wakitazamia kuandamama kwa mwezi,Mufti wa Tanzania Sheikh Abubakar Zuberi ametangaza kwa waislamu wote kuendelea mfungo wa mwezi mtukufu wa ramdahani kwa siku ya kesho jumapili ili kutimiza siku 30 za mwezi huu.

Mufti huyu anayewakilisha Baraza la waislamu Tanzania (BAKWATA) ametangaza hivyo leo kupitia vyombo vya habari majira ya saa mbili usiku,kuwa wamejaribu kuuliza na kutazama sehemu zote za tanzania na nchi za jirani ila hakuna sehemu iliyothibitisha kuuona mwezi huo.

Waislamu usheherekea sikuu hii baada ya kufunga mwezi wa Ramadhani kwa kutimiza siku 29 endapo watauona mwezi au kukamilisha siku 30 ikiwa hawakuuna mwezi.

Share :

Facebook Twitter Google+
0 Comments "WAISLAM KUSHEHEREKEA SIKUKUU YA IDD EL FITRI JUMATATU"

Back To Top