RAIS MAGUFULI ATUA KIBAHA LEO KUZINDUA VIWANDA 200

Rais John Pombe Joseph Magufuli amewasili leo  Kibaha bwawani mkoani Pwani kwa ajili ya uzinduzi wa viwanda zaidi ya 200 ambavyo vilianza kujengwa kabla na wakati huu wa utawala wake.

Viwanda hivyo 200 ambavyo vitakuwa eneo la kibaha vitazinduliwa na Rais Magufuli ktk ziara yake ya siku tatu ndani ya mkoa huo ikiwa ndio ziara yake ya kwanza toka kuaingia kwake madarakani novemba 2015.

Baadhi ya viwanda vitakavyozinduliwa na Rais Magufuli ni vile vya TAMCO,Global packaging,Kiluwa steel group,Elven Agric company,Sayona Fruits.

Rais pia atazindua mradi wa maji wa ruvu na barabara ya Bagamoyo Msata.

Rais atalala ndani ya ikulu ndogo ya Kibaha kwa siku mbili na siku ya tatu atakuwa anahitiumisha zaira hiyo ktk kuimarisha itikadi yake ya Tanzania ya viwanda.

Mda huu wa Saa tisa amewasili eneo la tukio kibaha bwawani.






Share :

Facebook Twitter Google+
0 Comments "RAIS MAGUFULI ATUA KIBAHA LEO KUZINDUA VIWANDA 200"

Back To Top