JE WAJUA KUWA MTUMIAJI WA VYAKULA VYA MBOGA MBOGA,NAFAKA NA MATUNDA KWA WINGI ANAKUWA SALAMA ZAIDI KIAFYA KULIKO ANAYETUMIA VYAKULA VITOKANAVYO NA WANYAMA!!!?


Mtu anyetumia mbogamboga na matunda kama kuwa sehemu ya vyakula vyake kwa asilimia 100% bila kugusa anaweza kuwa salama zaidi kiafya hasa ktk kuzeeka ama kufa mepema kutokana na magonjwa!



Ktk nchi kama Japan,China,korea na nyingine nyingi za watu wa Asia wao ndio watu waoongoza kwa kuishi kwa mda mrefu sana ktk dunia kuliko watu wengine.


Aina hii ya chakula unaweza kuwa bora na ina maana ikiwa tu zitapikwa au kutumia ustadi wa hali juu ili kuepuka kupoteza uhalisia wake.




Vyakula hivi hata kama vitalika kwa kiasi kikubwa na mlaji mara kwa Mara bado havitaweza kumletea mlaji hiyo aina yeyote ya madhara kwa Afya yake zaidi ya kuwa bora kiafya.
Vyakula vitokanavyo na wanyama,samaki na ndege wa aina mbalimbali vinatakiwa kutumia kwa kiasi kidogo sana kwa mwanadamu ktk mlo wake kwani vina kiasi kikubwa sana cha mafuta ambacho kikiliwa kwa wingi kinaweza kuleta madhara makubwa ya kiafya kwa malaji haswa kwa kumsababishia magonjwa kama unene uliopindukia,shinikizo la damu,kisukari.




Tambua kuwa vyakula vya mboga mboga,matunda na nafaka pia kiasi cha virutubisho vinavyopatikana wanyama,ndege na samaki,ambayo virutubisho hivyo havina kiasi kikubwa cha mafuta ya rehemu (Chelesterol) ukilinganisha na vile vinavyopatikana ktk wanyama.

Zingatia: Mwanadamu anaweza kuishi akiwa na Afya bora kabisa hata ikiwa atatumia vyakula vya mbogamboga,matunda na nafaka bila kugusa vyakula vya wanyama.

Ila haiwezekani kabisa mwanadamu akawa salama kiafya kwa kutumia vyakula hivyo vya wanyama pekee bila kugusa nafaka,matunda na mbogamboga









Share :

Facebook Twitter Google+
0 Comments "JE WAJUA KUWA MTUMIAJI WA VYAKULA VYA MBOGA MBOGA,NAFAKA NA MATUNDA KWA WINGI ANAKUWA SALAMA ZAIDI KIAFYA KULIKO ANAYETUMIA VYAKULA VITOKANAVYO NA WANYAMA!!!?"

Back To Top