MUHONGO ANYOFOLEWA TENA KTK UWAZIRI WA NISHATI NA MADINI

Ripoti ya uchunguzi wa makontena yaliyobeba mchanga ulisemekena una kiwango kikubwa cha madini ya dhahabu,shaba,aluminiam na mengine mengi kupelekwa nchi za ulaya.

Wamiliki wa migodi hiyo inayofanya kazi ya kuchimba mchanga huo kwa miaka mingi wamekuwa wakikanusha kuwa wanasafirisha mchanga wenye kiwango kikubwa cha madini bali wanapeleka mchanga huo kwa ajili ya kuyeyusha madini machache tu baada ya kukosekana kwa kiwanda na mitambo ya kuyeyushia aina hiyo ya madini nchini ambayo uhitaji zaidi ya nyuzi joto 1500 na kuendelea.

Kashfa hii iliibuka baada ya Mh.Rais kutembelea bandari ya  Dar es salaam ghafla na kuagiza kontena zaidi ya 20 kutosafirishwa kwenda popote pale mpaka hapo uchunguzi wa tume zaidi ya tatu alizoziunda Rais kukamilisha uchunguzi wake.

Leo ikulu saa tatu asubuhi ndion ilikuwa siku ya kukabidhiwa ripoti hiyo rasmi kwa Mh. rais na walioagizwa kufanya hivyo waliwasilisha ripoti hiyo iliyotoa uozo huo wa kilichomo ndani ya makontena ya michanga kuwa asilimia kubwa ya mchanga huo uligundulika na kukutwa na kiwango kingi cha madini ya thamni ya mabilioni ya dola za kimarekani.

Ripoti hiyo iliwaweka midomo wazi Mh Rais,waziri mkuu na makamu wa Rais wakati wakisikiliza kwa kusikia kiwango kikubwa cha mali za watanzania zilizokuwa zikipotea bila ya wao kujua.

Hali hii imelamzimisha Rais kumwagiza waziri wa nishati na madini Mh.Sospeter Muhongo kuwa akae na atazame kwa kujitathimini kwa kina na makini kama bado anafaa kukaa ktk cheo hicho,hii imetokana na kauli yake ya awali ya kiongozi huyu kuwa mchanga ule haukuwa na kiwango kikubwa cha madini kama watu walivyokuwa wakisema.

Mda mchache baada ya tangazo hilo waziri Sospeter Muhongo amemwandikiwa Mh.Rais barua kuwa ameamua kuachia ngazi kwa cheo hiko,hata hivyo Rais na alijibu barua hiyo kwa haraka leoleo kuwa ameridhia ombi lake hilo.

Idadi hii inafanya kufanya mawaziri walioondolewa kazini kufikia watatu baada ya Charles Kitwanga,Nape Nnauye toka kuwekwa kwa baraza la mawaziri ktk utwala wa Mh. Magufuli.







Waziri Sospeter Muhongo akiwa na Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania mh. John Pombe Magufuli


















Share :

Facebook Twitter Google+
0 Comments "MUHONGO ANYOFOLEWA TENA KTK UWAZIRI WA NISHATI NA MADINI"

Back To Top