JENGO LA GHOROFA 120 LAUNGUA MOTO KWA SAA 12 LONDON

"Nina ujuzi na ufanisi wa kuafnya kazi ya kuzima moto kwa miaka 29 sasa ila sijawahi kukutana na moto wa ajabu kama huu" Alisika mmoja wa wataalam wa zima moto walikuwepo ktk eneo la jengo linaloungua moto ktk mtaa wa latimer ktk nji wa Notting hill huko london magharibi.

jengo hili lenye ghorofa zipatazo 120 zilizohifadhi zaidi ya watu 600 lilishika moto leo asubuhi mapema ktk moja ya fleti ya mkaazi mmoja na kuhisiwa kuwa moto huo ulisababishwa na mlipuko wa friji iliyokuwa ikifanya kazi na kusababisha mtungi wa gasi kulipuka na kuleta moto mkali uliotapakaa haraka ktk ghorofa nyingine.

Watu 6 wameripotiwa kufa,20 wako hospitali ktk hali mahututi wakioata matibabu na zaidi ya 74 wakiwa wamepata majeraha ya moto wakiendelea kupata matibabu.

Jengo hili lenye mgawanyiko wa fleti 120 limegharimu zaidi ya pesa ya pound ya uingereza zaidi ya paundi milioni 10 sawa na pesa za kitanzania shilingi bilioni 3 na zaidi.

Moto huu ni mkubwa na makali zaidi uliosambaa kwa haraka kabisa kutokana na umeme na mifumo ya gesi iliyokuwemo ndani ya jengo hilo kubwa kabisa,bado hakuna taarifa zozote zilizohusisha moto huo na matukio ya kiahafu au kigaidi.




Share :

Facebook Twitter Google+
0 Comments "JENGO LA GHOROFA 120 LAUNGUA MOTO KWA SAA 12 LONDON"

Back To Top